Obama: Clinton anafaa zaidi kuwa rais Marekani
Rais wa Marekani Barack Obama
amemsifu sana mgombea wa chama cha Democratic Hillary Clinton na kusema
ndiye afaaye zaidi kuongoza Marekani.
Akihutubu katika kongamano
kuu la chama cha Democratic mjini Philadelphia, huku akishangiliwa na
wajumbe, Rais Obama amesema hakujawahi kuwa na mtu aliyehitimu zaidi
kuongoza Marekani kuliko Bi Clinton."Hakujawahi kuwa na mwanamume au mwanamke, iwe mimi au Bill Clinton au mtu mwingine yeyote aliyekuwa amehitimu zaidi kuwa rais kama yeye," amesema Bw Obama.
Amemsifu pia kwa kujikakamua na kuwa mwanamke wa kwanza katika historia ya taifa hilo kuteuliwa kuwa mgombea urais wa chama kikubwa.
Amempongeza kwa kubomoa vizuizi na kuunda nafasi zaidi kwa Wamarekani.
Amewaahidi Wamarekani kwamba Bi Clinton anatetea umoja na maadili ya Wamarekani.
Post a Comment